Wednesday, August 29, 2018

IJUE TANZANIA

Tanzania ni nchi iliyoko Afrika ya Mashariki
Imepakana na Uganda na Kenya upande wa kaskaziniBahari Hindi upande wa masharikiMsumbijiMalawi na Zambia upande wa kusiniKongoBurundi na Rwanda upande wa magharibi.
Eneo lina kilometa za mraba 947,303 (nchi ya 31 duniani); maji ya ndani yanachukua asilimia 6.2.
Idadi ya watu kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 ilikuwa 44,928,923 (nchi ya 30 duniani) kutoka 34,443,603 waliohesabiwa katika sensa ya mwaka 2002.
Msongamano ni wa watu 47.5 kwa km2 (nchi ya 124 duniani).
Tanzania ni nchi kubwa zaidi kati ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
Mji mkuu ni Dodoma (wenye wakazi 410,956), lakini rais bado yupo Dar es Salaamjiji kubwa zaidi, lenye watu zaidi ya milioni 4,364,541. 
Miji mingine ni kama vile Mwanza (706,543), Arusha (416,442), Mbeya (385,279), Morogoro (315,866), Tanga (273,332), Kahama (242,208), Tabora (226,999) na Zanzibar (223,033).
SOURCE WIKIPEDIA

No comments:

Post a Comment